UJERUMANI YAPUNGUZA UHUSIANO WAKE NA KOREA KASKAZINI.

TAREHE 01-12-2017




Ujerumani imepunguza uhusiano wake wa kibalozi na Korea Kaskazini baada ya nchi hiyo kufanya jaribio jingine la kombora la masafa marefu.

Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani, Sigmar Gabriel amesema akiwa ziarani nchini Marekani kwamba afisa mmoja wa kibalozi atapunguzwa kutoka kwenye ubalozi wa Ujerumani mjini Pyongyang.

Waziri Gabriel pia ameitaka Korea Kaskazini nayo ipunguze idadi ya wawakilishi wake wa kibalozi waliopo nchini Ujerumani.

Balozi wa Marekani kwenye Umoja wa Mataifa, Nikki Haley amezitaka nchi zote zivunje uhusiano wao wa kibalozi na Korea ya Kaskazini.
Pamoja na hayo Marekani imetishia kuuteketeza utawala wa Kim Jong Un endapo vita vitatokea.


Jumatano iliyopita Korea Kaskazini ilirusha kombora jipya ambalo linaweza kuifikia nchi yote ya Marekani.
UJERUMANI YAPUNGUZA UHUSIANO WAKE NA KOREA KASKAZINI. UJERUMANI YAPUNGUZA UHUSIANO WAKE NA KOREA KASKAZINI. Reviewed by safina radio on December 01, 2017 Rating: 5

No comments