WABUNGE WA REPUBLICAN NCHINI MAREKANI WAKUMBWA NA KIZINGITI.
20-12-2017

Wabunge wa
Republican nchini Marekani wamekumbwa na kizingiti cha dakika ya mwisho katika
juhudi zao za kuidhinisha marekebisho makubwa ya kodi kuwahi kufanywa katika
miaka 30, na hivyo wanahitaji kupiga kura tena hii leo,ingawa itachelewesha
kile ambacho kingekuwa ni ushindi wa kwanza kabisa bungeni chini ya Rais Donald
Trump.
Bunge la Marekani
ambalo linadhibitiwa na Warepublican lilipitisha mpango wa kodi jana na
kuuwasilisha mswada huo katika baraza la Seneti, ambako afisa mmoja alitoa
uamuzi kuwa vipengele vitatu vya mswada huo wa Bunge havikukidhi sheria pana za
Seneti.
Kufikia jana jioni,
mpango ulikuwa ni Seneti kufuta vipengele hivyo vitatu na kuupigia kura mswada
huo,ambapo Ikiwa utaidhinishwa kama inavyotarajiwa, mswada huo utarejeshwa Bungeni ili kupigiwa tena kura siku
ya leo.
WABUNGE WA REPUBLICAN NCHINI MAREKANI WAKUMBWA NA KIZINGITI.
Reviewed by safina radio
on
December 20, 2017
Rating:
No comments