MWANASIASA WA CHAMA CHA DEMOCRATS NCHINI MAREKANI APATA USHINDI MKUBWA

TAREHE 13-12-2017
Democratic Alabama U.S. Senate candidate Doug Jones and wife Louise acknowledge supporters at the election night party in Birmingham, Alabama, U.S., December 12, 2017.Haki miliki ya pichaREUTERS
Image caption
Mwanasiasa wa chama cha Democrats nchini Marekani Doug (Dag) Jones amepata ushindi mkubwa leo katika kinyang'anyiro kikali cha kuwania kiti cha Seneti katika jimbo la Alabama.

Jimbo hilo lilishikiliwa kwa muda mrefu na chama cha republican na ushindi wa Bw Jones ni pigo kwa rais wa Marekani Donald Trump .
Roy Moore wa Republican alishindwa kwa kupata asilimia 48.4 ya kura huku mgombea wa Demokrat akiibuka na ushindi kwa kupata kura asilimia 49.9.


Jones mwenye umri wa miaka 63 alikuwa mwendesha mashtaka wa serikali aliyepata umaarufu baada ya kuwashtaki wanachama wa kundi la imani kali ya kibaguzi Ku Klux Klan lililoshambulia kanisa moja la watu weusi katika miaka ya 1960 ambapo wasichana wanne waliuwawa.
MWANASIASA WA CHAMA CHA DEMOCRATS NCHINI MAREKANI APATA USHINDI MKUBWA MWANASIASA WA CHAMA  CHA DEMOCRATS NCHINI MAREKANI APATA  USHINDI MKUBWA Reviewed by safina radio on December 13, 2017 Rating: 5

No comments