WAFUGAJI MJINI SHINYANGA WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA ZA UFUGAJI YA MWAKA 2004.
TAREHE 19-12-2017
Wafugaji mjini
Shinyanga wametakiwa kuzingatia sheria za ufugaji ya mwaka wa 2004 ambayo
inaelekeza kufuga kwa kutumia mazizi vinginevyo watakaokiuka watachukuliwa
hatua za kisheria.
`
Kauli hiyo
imetolewa na afisa mifugo wa halmashauri ya Manspaa ya Shinyanga Bw Virwan
Mwaliko kufuatia mifugo kuzagaa mitaani na kusababisha uharibifu wa miundombinu
ya barabara.
Bw Mwaliko amesema
kuwa kwa mujibu wa sheria ya mifugo ya mwaka wa 2004 inasema kuwa mfugaji
atakayekiuka sheria hiyo atashtakiwa na adhabu yake ni kwenda jela miaka miwili
au kulipa faini ya shilingi elfu 50 au vyote kwa pamoja.
Hata hivyo afisa
huyo ameongeza kuwa katika kipindi cha miezi mitatu kuanzia mwezi Octoba hadi
Disemba mwaka huu jumla ya wafugaji mia moja na tano wamekamatwa na kutozwa
faini kwa mujibu wa sheria iliyowekwa.
WAFUGAJI MJINI SHINYANGA WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA ZA UFUGAJI YA MWAKA 2004.
Reviewed by safina radio
on
December 19, 2017
Rating:

No comments