MAKAMU WA RAIS WA TANZANIA SAMIA SULUHU HASSAN AHAMIA RASMI MJINI DODOMA.
TAREHE 15-12-2017
Makamu wa rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania
Mh Samia Suluhu Hassan leo amehamia rasmi mjini Dodoma ikiwa ni mkakati wa serikali
ya awamu ya tano ya kuhamishia shughuli zake mkoani humo ambako ndiko makao
makuu ya nchi.
Akizungumza mara baada ya kuwasili mkoani humo mjini
humo Mh Suluhu amesema kuwa kwa sasa shughuli zote za makamu wa rais muungano
na mazingira zitafanyikia mkoani Dodoma kwa
kuwa mawaziri wote wa wizara yake walikuwa ameshatangulia kufika katika makao
makuu hayo.
Ameongeza kuwa kwa kuwa ofisi yake inahusika na
mambo ya mazingira wameanza kampeni maalumu ya kuufanya mkoa wa Dodoma kuwa wa
kijani wa kupanda miti,ambapo kampeni hiyo itazinduliwa Disemba 21 mwaka huu na
kuwashirikisha wananchi wote wa mkoa huo.
Kwa upande wake waziri mkuu wa jamuhuri ya muungano
wa Tanzania Mh Majaliwa Kassimu Majaliwa amesema kuwa serikali inaendelea kuboresha miundombinu mbalimbali
ya mji wa Dodoma ikiwemo barabara na amewataka viongozi pamoja na wananchi
kushirikiana serikali katika sekta ya maendeleo ili kuhakikisha manspaa ya Dodoma inakuwa jiji kubwa hapa nchini.
Hata hivyo mbali na makamu wa rais viongozi wengine
ambao wameshahamia mjini Dodoma ni waziri mkuu Mh Majaliwa Kassimu,mawaziri wa
wizara zote,makatibu wakuu pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa taasisi
mbalimbali za serikali,ambapo rais Magufuli anatarajiwa kuhamia mjini humo
mapema mwakani.
MAKAMU WA RAIS WA TANZANIA SAMIA SULUHU HASSAN AHAMIA RASMI MJINI DODOMA.
Reviewed by safina radio
on
December 15, 2017
Rating:

No comments