WATOTO 4 WAFARIKI KATIKA AJALI NCHINI UFARANSA

TAREHE 15-12-2017
Ajali hiyo ilitokea karibia na eneo la shule
Image caption
watoto wanne wamefariki dunia huku wengine 20 wakijeruhiwa baada ya basi lao la shule kugongana na treni kusini magharibi mwa Ufaransa.


Vyombo vya habari nchini humo vimeripoti kuwa ajali hiyo imetokea kwenye eneo la makutano ya reli na barabara katika mji ulioko jirani na eneo la mpaka kati ya Ufaransa na Uhispania.

Watoto hao walio na umri kati ya miaka 11 na 17 walikuwa wakirejea nyumbani kutoka shule iliyoko jirani na mji wa Pepinan.



 Waziri Mkuu wa Ufaransa, Edward Philipe amesema uchunguzi kuhusiana na chanzo cha ajali hiyo bado unafanyika.
WATOTO 4 WAFARIKI KATIKA AJALI NCHINI UFARANSA WATOTO 4 WAFARIKI KATIKA AJALI NCHINI UFARANSA Reviewed by safina radio on December 15, 2017 Rating: 5

No comments