NIGERIA KUMBADILISHA KAMANDA WA JESHI ANAYEONGOZA VITA DHIDI YA BOKO HARAM

TAREHE 07-12-2017

Serikali ya Nigeria imeamua kumbadilidhsa kamanda wa jeshi anayeongoza vita dhidi ya kundi la kigaidi la Boko Haram ikiwa imepita nusu mwaka tu tangu ateuliwe kushika nafasi hiyo.

Msemaji wa jeshi la Nigeria amethibitisha habari hiyo na kuongeza kuwa, wimbi la mashambulizi ya magaidi wa Boko Haram limeongezeka sana hivi sasa, hivyo jeshi limeamua kumbadilisha kamanda aliyekuwa anaogoza vita dhidi ya genge hilo.
Amesema kuwa Makamanda wa kijeshi huwa wanabadilishwa mara kwa mara kama njia ya kutoa msukumo mpya katika vita dhidi ya ugaidi kwenye eneo la kaskazini mashariki mwa Nigeria ambapo uasi wa genge la wakufurishaji la Boko Haram umeingia katika mwaka wake wa tisa.


Hata hivyo kuzuka wimbi jipya la mashambulizi ya Boko Haram kunaonesha namna Rais Muhammadu Buhari wa Nigeria alivyoshindwa kutekeleza ahadi zake alizozitoa wakati wa kampeni za uchaguzi wa rais.
NIGERIA KUMBADILISHA KAMANDA WA JESHI ANAYEONGOZA VITA DHIDI YA BOKO HARAM NIGERIA  KUMBADILISHA KAMANDA WA JESHI ANAYEONGOZA VITA DHIDI YA BOKO HARAM Reviewed by safina radio on December 07, 2017 Rating: 5

No comments