JITIHADA YA KUTOA ELIMU ZAIDI YA KUJIKINGA NA MAGONJWA KABLA YA KUUGUA YAHITAJIKA.



TAREHE 19-12-2017.


Katibu mkuu wizara ya afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Dr Mpoki Wilisibisya amezitaka taasisi na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali yanayojihusisha na masuala ya afya kuweka jitihada ya kutoa elimu zaidi ya kujikinga na magonjwa kabla ya kuugua.

Dr Willsibisya ameyasema hayo mkoani Geita wakati wa makabidhiano ya vifaa vya watoto njiti vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 14 iliyotolewa na kampuni ya Vodacom Foundation hapa nchini katika hospitali ya Chato mkoani Geita.

Amesema kuwa endapo elimu itatolewa kwa wananchi namna ya kujikinga na magonjwa mbalimbali itasaidia kuokoa gharama za matibabu pamoja na kuokoa nguvu kazi ya taifa kwa kuwa mtu akiugua kasi yake ya kufanya kazi inapungua na kinga ni bora kuliko tiba.

Kwa upande wake mganga mfawidhi wa hospitali hiyo Dr Ligibati Kausa amesema kuwa,upatikanaji wa vifaa hivyo utasaidia watoto katika kuwahudumia kiundani zaidi kwa kuwa watakuwa wamezaliwa kabla ya wakati.
JITIHADA YA KUTOA ELIMU ZAIDI YA KUJIKINGA NA MAGONJWA KABLA YA KUUGUA YAHITAJIKA. JITIHADA YA KUTOA ELIMU ZAIDI YA KUJIKINGA NA MAGONJWA KABLA YA KUUGUA YAHITAJIKA. Reviewed by safina radio on December 19, 2017 Rating: 5

No comments