RAIS DONALD TRUMP WA MAREKANI APATA USHINDI MAHAKAMANI.

TAREHE 05-12-2017


Rais Donald Trump wa Marekani amepata ushindi baada ya majaji wa mahakama ya juu nchini humo kuamua amri ya marufuku yake ya hivi karibuni dhidi ya wasafiri kutoka mataifa sita yaliyo na Waislamu wengi kuanza kutekelezwa rasmi.

Mahakama imebatilisha mapingamizi yaliyokuwa yamewekwa na mahakama za chini ambayo kwa kiasi fulani yalizuia utekelezaji wa amri hiyo.
Marufuku hiyo ya muda inayalenga mataifa ya Iran, Libya, Syria, Yemen, Somalia na Chad huku Korea Kaskazini na baadhi ya maafisa kutoka Venezuela wakiongezwa katika orodha ya sasa.


Amri hiyo ya Trump ilikosolewa huku baadhi ya mahakama nchini Marekani zikiamua kuwa Trump hawezi kuwazuia walio na mahusiano na watu nchini Marekani kutoingia nchini humo.
RAIS DONALD TRUMP WA MAREKANI APATA USHINDI MAHAKAMANI. RAIS DONALD TRUMP WA MAREKANI APATA USHINDI MAHAKAMANI. Reviewed by safina radio on December 05, 2017 Rating: 5

No comments