BARAZA LA JUU LA TAIFA NCHINI LIBYA LAPATA MWENYEKITI.


Baraza la Juu la Taifa la Libya jana lilipiga kura na kumchagua Bw. Khaled al-Meshri kutoka Chama cha Haki na Ujenzi kuwa mwenyekiti mpya wa Baraza hilo akichukua nafasi ya Bw. Abdarrahman Swehli.


Duru za habari zinaeleza kuwa baraza hilo ni chombo cha kutoa ushauri kwa serikali ya umoja wa kitaifa ya Libya inayotambuliwa na jumuiya ya kimataifa.

Mjumbe wa Baraza hilo Bw. Musa Faraj amesema kuwa kwa mujibu wa kanuni, mwenyekiti wa Baraza hilo anachaguliwa kila mwaka.

Hata hivyo, wajumbe mia moja kumi na tano wa Baraza hilo walipiga kura na Bw. Khaled al-Meshri alipata kura sitini na nne ambazo ni kura kumi na tisa zaidi kuliko Bw. Swehli, na wajumbe wengine sita hawakupiga kura.


BARAZA LA JUU LA TAIFA NCHINI LIBYA LAPATA MWENYEKITI. BARAZA LA JUU LA TAIFA NCHINI LIBYA LAPATA MWENYEKITI. Reviewed by safina radio on April 09, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.