GUTERRES AMTEUA MEJA JENERALI GEBRE ADHANA WOLDEZGU KUWA KAMANDA UN HUKO ABYEI.


Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw Antonio Guterres ametangaza kumteua Meja Jenerali Gebre Adhana Woldezgu kutoka Ethiopia kuwa kamanda mpya wa tume ya Umoja wa Mataifa huko Abyei, eneo linalogombewa kati ya Sudan na Sudan Kusini.

Image result for Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw Antonio Guterres
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw Antonio Guterres.
Bw Guterres amesema Bw Gebre ana uzoefu wa miaka 38 katika jeshi la Ethiopia, na amewahi kwenda mara kwa mara Sudan, Sudan Kusini, Kenya, Uganda na tume ya Umoja wa Mataifa nchini Somalia, kwa ajili ya kuimarisha uratibu wa mambo ya usalama na mipaka wakati akizungumza na wanahabari.

Aidha, Bw Gebre amechukua nafasi ya Meja Jenerali Tesfay Gidey Hailemichael wa Ethiopia, ambaye amesifiwa kutoa mchango mkubwa kwa tume hiyo.

Hata hivyo, amewahi kushiriki kwenye kazi ya upangaji wa operesheni za kulinda amani za kimataifa na za kikanda.

GUTERRES AMTEUA MEJA JENERALI GEBRE ADHANA WOLDEZGU KUWA KAMANDA UN HUKO ABYEI. GUTERRES AMTEUA MEJA JENERALI GEBRE ADHANA WOLDEZGU KUWA KAMANDA UN HUKO ABYEI. Reviewed by safina radio on April 05, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.