BURUNDI YASHUTUMU RWANDA NA UNHCR KWA UTEKAJI NYARA WA WAKIMBIZI WAKE.

Image result for burundi flag





Serikali ya Burundi imeishutumu Rwanda na wafanyakazi wa Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR kwa kuwateka nyara wakimbizi wa Burundi     
        
Msemaji wa serikali ya Burundi Bw. Philippe Nzobonariba ametoa taarifa ya kuihimiza Rwanda kuwaachia huru na kuwarejesha wakimbizi wanaoshikiliwa mateka na serikali ya Rwanda kwa kushirikiana na wafanyakzi wa ofisi ya Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa nchini Rwanda.

Taarifa hiyo imetolewa baada ya kurejeshwa kwa takriban wakimbizi 2,500 kutoka kambi tatu za mpito nchini Rwanda wikiendi iliyopita.

Hata hivyo, mwishoni mwa mwezi Machi, wizara ya mambo ya maafa na wakimbizi ya Rwanda imesema wakimbizi zaidi ya 2,500 wa Burundi walioingia Rwanda kutoka kambi moja ya DRC, watarejeshwa Burundi kuanzia mwanzoni mwa Mwezi huu.

BURUNDI YASHUTUMU RWANDA NA UNHCR KWA UTEKAJI NYARA WA WAKIMBIZI WAKE. BURUNDI YASHUTUMU RWANDA NA UNHCR KWA UTEKAJI NYARA WA WAKIMBIZI WAKE. Reviewed by safina radio on April 05, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.