WHITE HOUSE YASEMA JESHI LAKE HAINA MUDA RASMI WA KUONDOKA SYRIA.


Ikulu ya Marekani White House imesema kuwa hakuna muda rasmi uliopangwa kwa vikosi vya nchi hiyo kuondoka nchini Syria, ingawa rais wa Marekani ameonyesha nia ya kuondoa haraka jeshi la nchi hiyo nchini Syria.

Image result for Ikulu ya Marekani White House
Ikulu ya White House.
Msemaji wa ikulu ya Marekani Sarah Sanders amesema, rais Donald Trump wa nchi hiyo anaangalia uwezekano wa kushinda vita hiyo kihalisi, na sio kuweka idadi kubwa ya askari nchini Syria.

Wakati huohuo, wizara ya ulinzi ya Marekani na wizara ya mambo ya nje ya nchi hiyo zimeeleza wasiwasi wao kuwa juhudi za muda mrefu zinahitajika ili kulishinda kikamilifu kundi la wapiganaji la IS.

Hata hivyo, mpaka sasa, jumla ya askari 2,000 wa Marekani wako nchini Syria.

WHITE HOUSE YASEMA JESHI LAKE HAINA MUDA RASMI WA KUONDOKA SYRIA. WHITE HOUSE YASEMA JESHI LAKE HAINA MUDA RASMI WA KUONDOKA SYRIA. Reviewed by safina radio on April 05, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.