JAMII IMESHAURIWA KUTAMBUA KUWA HOFU NA MASHAKA NI DALILI YA VIFUNGO
Jamii imeshauriwa kutambua kuwa mtu mwenye hofu na
mashaka ya kufanya jambo lolote la kimaendeleo katika maisha yake au kutokuwa
na kiu ya kusoma na kutafakari neno la Mungu ni mojawapo kati ya dalili za mtu
aliyekamatwa na kufungwa vifungo vingi na mwovu shetani.
Huduma ya redio safina kesho katika ukumbi wa maombi
uliopo mbauda jijini Arusha kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa sita mchana
imekuandalia maombi maalum ya kuwafungua watu waliofungwa na vifungo mbalimbali
ambavyo vimekuwa sababu za wao kutokufikia Baraka walizowekewa na Mungu.
Kwa mujibu wa somo la kesho la kushughulikia vifungo
vilivyowafunga watu wasifanikiwe, majira na nyakati za mtu zinaweza kufungwa na
shetani ili mtu huyo asiweze kufikia mafanikio yake katika nyanja mbalimbali
ikiwemo elimu,afya,kilimo,baishara,ufugaji, pamoja na huduma kwa ujumla.
somo hilo linaeleza kuwa shetani amekuwa
akifuwanga watu hasa katika eneo la uchumi,na kuachilia
madeni,magonjwa,majeraha ya ndoa, watoto kuacha shule,lakini mtu anapojikita
kwenye maombi kwa kutumia neno la Mungu vifungo hivyo hufunguliwa na mtu
kuwekwa huru.
Hata hivyo kesho ni siku ya watu kufundishwa jinsi
ya kulituma neno la Mungu ili kufungua fungo vyote vinavyowazuia wasiweze
kuinuka kiuchumi na kiroho ambapo watu wenye mahitaji mbalimbali wataombewa ili
Mungu awaweke huru mbali na vifungo vya shetani.
JAMII IMESHAURIWA KUTAMBUA KUWA HOFU NA MASHAKA NI DALILI YA VIFUNGO
Reviewed by safina radio
on
April 09, 2018
Rating:
No comments