SERIKALI YAANZA KUFUFUA VIWANDA VILIVYOBADILISHWA MATUMIZI.


Serikali kupitia wizara ya viwanda biashara na uwekezaji imeanza kufufua viwanda vilivyokuwa vimebadilishwa matumizi yake ili kurejesha shughuli za awali za viwanda hivyo.
Image result for PICHA YA STELLA MANYANYA NAIBU WAZIRI WA VIWANDA
STELLA MANYANYA 
Hayo yamesemwa leo bungeni mjini Dodoma na Naibu Waziri wa  viwanda biashara na uwekezaji Mhadisi Stella Manyanya wakati akijibu swali la mbunge wa Viti maalumu Mariamu Nassoro Kisangi aliyetaka kujua ni kwa nini baadhi ya viwanda vimebadilishwa matumizi yake na kuwa maghala ya kuhifadhia vifaa mbali mbali jijini Dar es salaam.

Mhandisi Manyanya amesema kuwa mpango wa serikali ni kuhamasisha na kuwezesha viwanda visivyofanya kazi viweze kufanya kazi ambapo uhamasishaji huo wa serikali umewezesha jumla ya viwanda  kumi na nane  kikiwemo kiwanda cha USI kilichokuwa kikitengeneza zana za kilimo ambacho kilibadilishwa matumizi na kuwa Tanzania Fillpipe LTD cha kutengeneza mabomba ya maji.

Aidha, amesema kuwa chini ya kamati maalumu wizara inaendelea kufuatilia utendaji wa viwanda hivyo vilivyofufuliwa kimoja baada ya kingine ili viweze kufanya kazi kwa tija.

Hata hivyo, viwanda mia moja hamsini na sita vilibinafsishwa kwa dhumuni la kutoa ajira, kuzalisha bidhaa zinazokidhi viwango vya kitaifa na kimataifa na kuongeza mchango wa viwanda katika uchumi wa taifa ikiwa ni miongoni mwa idadi ya mashirika ya umma mia tatu arobaini na moja yaliyobinafsishwa na serikali hadi kufikia mwaka 2007.

SERIKALI YAANZA KUFUFUA VIWANDA VILIVYOBADILISHWA MATUMIZI. SERIKALI YAANZA KUFUFUA VIWANDA VILIVYOBADILISHWA MATUMIZI. Reviewed by safina radio on April 09, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.