asilimia 27 ya vijana wa kike wenye umri kati ya miaka 15-19 hapa nchini wamepata ujauzito.
Naibu waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee
na watoto Mh Faustine Ndugulile amesema kuwa asilimia 27 ya vijana wa kike
wenye umri kati ya miaka 15-19 hapa nchini wamepata ujauzito.
NAIBU WAZIRI WA AFYA FAUSTINE NDUGULILE |
Mh Ndugulile ameyasema hayo leo bungeni mjini Dodoma
wakati akijibu swali la mbunge wa viti maalumu mkoa wa Singida Mh Asha Rose
Matende aliyetaka kujua serikali una mpango gani wa kupunguza mimba za utotoni
hapa nchini.
Amesema kuwa kutokana na takwimu hizo serikali kwa
kushirikiana na wadau mbalimbali wa elimu wameanzisha kampeni maalumu inayomwahamasisha
msichana kujitambua inayokwenda kwa jina la “Mimi ni Msichana Najitambua Elimu
ndio Mpango Mzima”.
Amefafanua kuwa mbali na kuanzisha kampeni hiyo
serikali pia imeanzisha utaratibu wa kutoa elimu kwa mikoa ambayo inaongoza kwa
mimba za utotoni ili wananchi wajue madhara yatokanayo na vitendo hivyo ikiwemo
vifo vitokanavyo na uzazi pale msichana atakapopata mimba aikiwa na umri mdogo.
Hata hivyo ili kukabiliana na matatizo ya uzazi kwa
wanawake katika mwaka wa fedha wa 2018/2019 serikali imetenga bajeti ya afya ya
uzazi kiasi cha shilingi bilioni 18 kutoka shilingi bilioni 5 za awali.
asilimia 27 ya vijana wa kike wenye umri kati ya miaka 15-19 hapa nchini wamepata ujauzito.
Reviewed by safina radio
on
April 10, 2018
Rating:
No comments