VIONGOZI WA VIJIJI WATAKIWA KUANZISHA MADAFTARI YA KUTUNZA KUMBUKUMBU


Jeshi la polisi Mkoani Rukwa limewataka viongozi wa serikali za vijiji kuanzisha madaftari ya kutunza kumbukumbu ya wakazi wa maeneo yao sanjari na wageni wanaoingia katika vijji vyao ili kupambana na vitendo vya kihalifu kwenye maeneo wanayoyaongoza.

Image result for PICHA YA KAMANDA WA POLISI MKOANI RUKWA GEORGE KIANDO
KAMANDA WA POLISI MKOA WA RUKWA GEORGE KIANDO

Wito huo umetolewa na kamanada wa polisi mkoani Rukwa Gorge Kiando kufuatia vitendo vya mauaji yaliyokuwa yakiongezeka katika maeneo yao hususani kwenye wilaya ya Sumbawanga kwenye bonde la ziwa Rukwa.

Aidha wananchi wa maeneo hayo wanawataka baadhi ya viongozi wa serikali za vijiji wanaokabiliwa na tuhuma hizo kubadili mienendo yao kwa kuacha tamaa za kutaka kujipatia fedha hizo haraka kwa kuwakumbatia wahalifu.

Mkoa wa Rukwa katika miaka ya hivi karibuni umekuwa ukiripotiwa vitendo vingi vya mauaji ya vikongwe ambazo zinatokana na tuhuma za vitendo vya kishirikina sanjari na visa vya wivu wa kimapenzi.

VIONGOZI WA VIJIJI WATAKIWA KUANZISHA MADAFTARI YA KUTUNZA KUMBUKUMBU VIONGOZI WA VIJIJI WATAKIWA KUANZISHA MADAFTARI YA KUTUNZA KUMBUKUMBU Reviewed by safina radio on April 10, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.