KIM JONG UN AZUNGUMZA KATIKA MKUTANO WA CHAMA TAWALA.


Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un amezungumzia hadharani kwa mara ya kwanza katika mkutano wa chama tawala katika mji mkuu wa nchi hiyo, Pyongyang.
Image result for PICHA YA KIM JONG UN

Rais wa Marekani alikubali mwezi uliopita kukutana na rais wa Korea Kaskazinii, mkutano ambao utakua wa kwanza katika historia kati ya rais wa Marekani madarakani na kiongozi wa Korea Kaskazini.
Katika mkutano wa maafisa waandamizi wa chama cha tawala, Bw Kim walijadili "maendeleo ya sasa kuhusu uhusiano wa Korea mbili na matarajio ya mazungumzo kati ya Marekani na Korea Kaskazini", shirika la habari la Korea Kaskazini la KCNA limearifu.
Kim Jong Un alitoa ripoti kuhusu hali inayoendelea katika rais ya Korea" na hasa mkutano mwingine, uliopangwa kufanyika mwishoni mwa mwezi huu pamoja na Korea Kusini, kwa mujibu wa shirika la habari la KCNA.
Trumple alitangaza mwezi uliopita kuwa alikubali mkutano na rais wa Korea Kaskazini kujadili uwezekano wa kuondoa silaha za nyuklia katika rasi ya Korea.




KIM JONG UN AZUNGUMZA KATIKA MKUTANO WA CHAMA TAWALA. KIM JONG UN AZUNGUMZA KATIKA MKUTANO WA CHAMA TAWALA. Reviewed by safina radio on April 10, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.