MAZUNGUMZO YA AMANI KUHUSU SUDANI KUSINI YANAANZA TENA KATIKA MJI MKUU WA ETHIOPIA ADDIS ABABA


Mazungumzo ya amani nchini Sudan Kusini yanaanza tena katika mji mkuu wa Ethiopia, Addis Abba.
Image result for PICHA YA RIEK MACHAR
RIEK MACHAR
 Mazungumzo hayo yanalenga kufikia amani ya kudumu na makubaliano ya kuachiliwa kwa aliye kuwa makamu wa rais Riek Machar, ambaye yuko katika kizuizi cha nyumbani nchini Afrika Kusini.
Mazungumzo hayo yanaanza wakati ambapo makundi mapya ya waasi yanaendelea kuundwa.
Aliyekuwa Mkuu Majeshi nchini humo Paul Malong ameunda kundi  jipya kundi la waasi,ambapo mkuu huyo alitimuliwa katika wadhifa wake na Rais Salva Kiir mwaka uliyopita, amechukua hatua hiyo dhidi ya utawala wa Kiir.
Malong ambaye amekuwa akiituhumu serikali kwa rushwa na makosa yamengine ya ufisadi, amesema kuwa kundi lake litakuwa na jukumu kubwa la kuiondoa Sudan Kusini kwenye sintofahamu na kuielekeza katika demokrasia na maendeleo.
Sudan Kusini imeendelea kukumbwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe. Vita hivyo vilianza mwaka mmoja tu baada ya taifa hilo changa kujipatia uhuru wake.

MAZUNGUMZO YA AMANI KUHUSU SUDANI KUSINI YANAANZA TENA KATIKA MJI MKUU WA ETHIOPIA ADDIS ABABA MAZUNGUMZO YA AMANI KUHUSU SUDANI KUSINI YANAANZA TENA KATIKA MJI MKUU WA ETHIOPIA ADDIS ABABA Reviewed by safina radio on April 10, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.