BARAZA LA USALAMA LA UMOJA WA MATAIFA KUPIGA KURA LEO.


Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa huenda likapiga kura mapema leo kuhusu maazimio kinzani ya Marekani na Urusi ya kuchunguza mashambulizi ya silaha za sumu nchini Syria, na hivyo kuanzisha mgongano ambao huenda ukachochea kutumiwa kura za turufu kupinga maazimio hayo yote.
Image result for PICHA YA SHAMBULIZI KATIKA MJI DOUMA NCHINI SYRIA

Marekani imewasilisha jana rasimu ya azimio kufuatia madai ya shambulizi la gesi ya sumu katika mji wa Douma unaodhibitiwa na waasi ambalo limewaua karibu watu 40 na kumfanya Rais Donald Trump kuashiria kuwa Marekani huenda ikachukuwa hivi karibuni uamuzi kuhusu hatua ya kijeshi. 
Urusi iliwasilisha pendekezo lake mwezi Januari ambalo limekataliwa na mataifa ya Magharibi yanayosema kuwa linaweza kuipa serikali ya Syria faida kubwa kuhusiana na uchunguzi unaofanywa ndani ya nchi.
Umoja wa Ulaya na nchi za Magharibi zinautuhumu utawala wa Rais wa Syria Bashar al-Assad, unaoungwa mkono na Urusi na Iran, kwa kufanya shambulizi hilo la sumu huku Urusi ikisema hakuna shambulizi lolote la sumu lililofanywa mwishoni mwa wiki.


BARAZA LA USALAMA LA UMOJA WA MATAIFA KUPIGA KURA LEO. BARAZA LA USALAMA LA UMOJA WA MATAIFA KUPIGA KURA LEO. Reviewed by safina radio on April 10, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.