WANADIPLOMASIA 60 WA MAREKANI WAFUKUZWA NCHINI URUSI
Wanadiplomasia 60 wa Marekani ambao wamefukuzwa kutoka Nchini
Urusi baada ya sakata la sumu inayodaiwa kupewa jasusi wa zamani Serguei
Skripal na binti yake wameondoka katika ubalozi wa Washington huko Moscow
mapema leo.
Mwandishi wa shirika la habari la AFP Alieyeko Moscow
ameshuhudia msafara wa mabasi matatu ya ubalozi wa Marekani pamoja na magari
mengine yakielekea kwenye uwanja wa kimataifa alfajiri ya leo
Hatua hiyo inakuja baada ya Moscow kuweka tarehe ya Aprili 5
kuwa tarehe ya mwisho kwa wanadiplomasia wa Marekani wawe wameshaondoka nchini
humo.
Wiki iliyopita Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Urusi, Sergei
Lavrov, amesema nchi yake itawafukuza nchini humo wanadiplomasia 60 wa Marekani
na kufunga ofisi za ubalozi wake mjini Saint Petersburg kujibu kitendo cha
wanadiplomasia wake kufukuzwa na nchi za Magharibi.
Utawala wa Washington wenyewe umesema kuwa kitendo kilichofanywa
na Urusi hakina msingi wowote na kwamba Serikali inafikiria hatua nyingine za
kuchukua.
WANADIPLOMASIA 60 WA MAREKANI WAFUKUZWA NCHINI URUSI
Reviewed by safina radio
on
April 05, 2018
Rating:
No comments