ZAIDI YA EKARI MILIONI MOJA ZA MITI HUVUNWA KILA MWAKA NCHI NA KULETA HOFU YA KUTOKEA KWA JNGWA.
Waziri wa Maliasili na Utalii Dk. Hamis Kigwangala
ameagiza Wakala wa Misitu Nchini TFS kuandaa tathmini ya uvunaji wa miti
itakayoonyesha kiwango cha misitu inayofaa kuvunwa ili kupunguza kasi ya
uvunaji wa misitu isiyokuwa na manufaa.
Waziri wa Maliasili na Utalii Dk. Hamis Kigwangala. |
Dk. Kigwangala ameyasema hayo wakati wa maadhimisho
ya kilele cha siku ya upandaji miti kitaifa yaliyofanyika wilayani Kishapu
Mkoani Shinyanga ambapo amesema kuwa zaidi ya ekari milioni moja huvunwa kila
mwaka hali inayotishia Taifa kugeuka kuwa jangwa endapo uvunaji huo
hautadhibitiwa.
Uvunaji misitu. Ukataji miti. |
Waziri Kigwangala ameungana na wakuu wa Mikoa ya
Shinyanga na Tabora katika maadhimisho hayo kwa kupanda miti katika eneo la
Hospitali ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga.
Aidha, kauli mbiu ya maadhimisho hayo ya siku ya
upandaji miti kitaifa mwaka huu yaliyofanyika mkoani humo ni Tanzania ya
viwanda inawezekana, panda miti kwa maendeleo ya viwanda.
ZAIDI YA EKARI MILIONI MOJA ZA MITI HUVUNWA KILA MWAKA NCHI NA KULETA HOFU YA KUTOKEA KWA JNGWA.
Reviewed by safina radio
on
April 05, 2018
Rating:
No comments