WAZIRI NDALICHAKO AIONYA TAMONGSCO KUTOAJIRI WALIMU KUTOKA NJE YA NCHI WASIO NA SIFA.
Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia na Mafunzo ya
Ufundi Prof. Joyce Ndalichako amewaonya wamiliki wa shule binafsi nchni ambao
wamekuwa wakiwaajiri walimu kutoka nje ya nchi wasiokuwa na vibali vya kuishi
nchini kufuata sheria za nchi.
Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Prof. Joyce Ndalichako. |
Waziri Ndalichako ameyasema hayo Mjini Dodoma wakati
akifungua Mkutano Mkuu wa Wamiliki na Mameneja wa Shule za Msingi na Sekondari
binafsi TAMONGSCO.
Aidha, Prof. Ndalichako ameongeza kuwa miongoni mwa
walimu hao wanaoajiriwa kutoka nje ya nchi wamebainika kukosa sifa za wizara ya
elimu na mafunzo ya ufundi hapa nchini.
Pia Mkutano
huo uliowakutanisha Wamiliki hao wa Shule Binafsi za Msingi na Sekondari
unajadili namna ya kuongeza kiwango cha ufaulu katika shule hizo.
Kwa upande wa baadhi ya wamiliki hao wameiomba
serikali kuwapunguzia kodi ili nao waweze kushusha ada kwa wazazi
wanaowasomesha watoto wao katika taasisi binafsi za elimu.
WAZIRI NDALICHAKO AIONYA TAMONGSCO KUTOAJIRI WALIMU KUTOKA NJE YA NCHI WASIO NA SIFA.
Reviewed by safina radio
on
April 05, 2018
Rating:
No comments