MAGUFULI AZINDUA UKUTA ULIOJENGWA NA JKT KATIKA MACHIMBO YA MERERANI MANYARA.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Magufuli amezindua ujenzi wa ukuta unaozunguka maeneo ya machimbo ya madini ya TANZANITE eneo la Mererani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara.

Image result for Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Magufuli

Dk. Magufuli amelipongeza jeshi la kujenga taifa JKT kwa kazi nzuri ya utekelezaji wa ujenzi wa mradi huo huku akiwahidi kuwaajiri katika nyanja mbali mbali za sekta ya ulinzi kutokana na kazi waliyoifanya.

Kwa upande wake, Waziri wa Madini Mh. Anjela Kairuki amesema kuwa kwa sasa Wizara madini imeanza kuandaa Kanuni na Taratibu za eneo hilo la Machimbo ya Madini ya TANZANITE Mererani Control Area, pamoja na taratibu nyinginezo ikiwemo vitambulisho vya wafanyakazi na uthaminishaji wa madini hayo.

Naye Waziri wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dk. Hussein Mwinyi amesema Jeshi hilo liko tayari kutekeleza maagizo yoyote ya serikali na utekelezaji wa miradi ya kitaifa kwa maendeleo ya nchi.

Hata hivyo lengo la ujenzi wa mradi wa ukuta huo wa Mererani katika  machimbo ya TANZANITE ni kudhibiti upotevu wa mapato ya ndani ya nchi.

MAGUFULI AZINDUA UKUTA ULIOJENGWA NA JKT KATIKA MACHIMBO YA MERERANI MANYARA. MAGUFULI AZINDUA UKUTA ULIOJENGWA NA JKT KATIKA MACHIMBO YA MERERANI MANYARA. Reviewed by safina radio on April 06, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.