HOMA YA LISSA YAUA MAKUMI YA WATU NCHINI NIGERIA.


ABUJA.
Wizara ya Afya ya Nigeria imetangaza kuwa makumi ya watu wamefariki dunia nchini humo kutokana na maambukizi ya homa ya Lassa.
Ugonjwa wa homa ya Lassa Afrika Magharibi unaelezwa kusahaulika kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola na Wahudumu wa afya wamesema huenda wakakosa rasilimali kukabiliana na ugonjwa huo iwapo utakithiri.
Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Afya ya Nigeria imesema kuwa, kesi 193 za maambukizi ya homa ya Lassa zimeshuhudiwa katika majimbo 17 ya nchi hiyo kwenye kipindi cha miezi miwili iliyopita na kwamba watu 43 wamefariki dunia kutokana na homa hiyo.
Taarifa hiyo imeongeza kuwa, idadi ya watu waliofariki dunia kutokana na homa hiyo ni sawa na asilimia 24 ya kesi zote zilizothibitisha  uwepo wa ugonjwa huo kote nchini Nigeria. 
Wakati huo huo Shirika la Afya duniani WHO limesema kuwa idadi mpya ya waathirika wa homa ya Lassa ambayo imetolewa na kituo cha kudhibiti magonjwa cha Nigeria-NCDC- inaonesha kuwa kati ya Januari Mosi na Februari 25 mwaka 2018, visa elfu moja na themanini vya homa ya Lassa viliripotiwa na kwamba watu 90 wamefariki dunia kutokana na ugonjwa huo. 
Wizara ya Afya ya Nigeria imesema kwa kawaida ugonjwa wa homa wa Lassa husambaa katika kipindi cha ukame lakini sasa unashuhudiwa katika vipindi na misimu yote ya mwaka.
Ugonjwa wa homa ya Lassa ulishuhudiwa kwa mara ya kwana nchini Nigeria mwaka 1969 katika mji wa Lasa na kwa sababu hiyo ulipewa jina la mji huo ambapo wataalam wanasema kuwa Ugonjwa huo unashabihiana sana na ule wa Ebola. 

HOMA YA LISSA YAUA MAKUMI YA WATU NCHINI NIGERIA. HOMA YA LISSA YAUA MAKUMI YA WATU NCHINI NIGERIA. Reviewed by safina radio on March 01, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.