MAHENGE AMTAKA MKANDARASI WA MRADI WA UMWAGILIAJI UNAOFADHILIWA NA WFP KUKAMILISHA MRADI HUO NDANI YA WIKI MBILI.


DODOMA.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dk. Bilinith Mahenge ametoa muda wa wiki mbili kwa mkandarasi wa mradi wa umwagiliaji maji unaofadhiliwa na Shirika la Chakula Duniani WFP kukamilisha mradi huo  uliotarajiwa kukamilika mwaka 2017 wilayani Chamwino.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dk. Bilinith Mahenge
Maelekezo hayo yametolewa katika ziara yake ya kutembelea na kukagua miradi ya kilimo inayotekelezwa wilayani Chamwino itakayogharimu zaidi ya fedha shilingi milioni 18 ambapo vijiji vitatu vinatarajia kunufaika na mradi huo.

Mkuu huyo wa mkoa amesema kuwa kwa muda uliobaki mkandarasi huyo hanabudi kupeleka mafundiwote katika eneo la mradi ili kuukmilisha kwa wakati mbali na changamoto zilizopo.

Hata hivyo, Dk. Mahenge amemwagiza na kumtaka mkandarasi huyo pamoja na mafundi wake wahakikishe wanatumia vizuri muda huo wa wiki mbili .
\




MAHENGE AMTAKA MKANDARASI WA MRADI WA UMWAGILIAJI UNAOFADHILIWA NA WFP KUKAMILISHA MRADI HUO NDANI YA WIKI MBILI. MAHENGE AMTAKA MKANDARASI WA MRADI WA UMWAGILIAJI UNAOFADHILIWA NA WFP KUKAMILISHA MRADI HUO NDANI YA WIKI MBILI. Reviewed by safina radio on March 05, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.