ZAIDI YA RAIA SABA WA ETHIOPIA WAMEKAMATWA MKOANI MWANZA.


MWANZA.

Zaidi ya wahamiaji haramu saba raia wa Ethiopia wamekamatwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kuingia nchini kinyume cha sheria.

Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Ahmed msangi.
Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Ahmed msangi amesema kuwa kukamatwa kwa watuhumiwa hao kunafuatia taarifa ya msamaria mwema aliyewatilia shaka na kutoa taarifa kwa jeshi la polisi juu ya uwepo wa watu kwenye kichaka katika eneo la Nyenyeshishi wilayani Misungwi.

Aidha, amesema kuwa walikuwa na taarifa kutoka kwa mtu huyo ambaye ni msamaria mwema  iliyopelekea kuagiza jeshi la polisi kufika maeneo hayo ya tukio ambapo  lilifanikiwa kuwakamata watu hao.

Pia, Kamanda Msangi ameongeza kuwa wahamiaji waliokamatwa ni raia tisa wa Ethiopia ambapo awali walikamatwa raia saba na baadae raia wawili walikamatwa katika eneo jingine tofauti na hilo walipokuwa  raia saba huku akidokeza kuwa wahamiaji hao  hawajui  lugha ya Kiswahili wala kingereza.

Hata hivyo, Kamanda Msangi ameongeza katika mahojiano kati ya Polisi na Wahamiaji, wahamiaji hao walikuwa wakitamka neno Ethiopia pekee kwa hiyo ni dhahiri kuwa waahamiaji hao ni raia wa Ethiopia.

Katika hatua nyingine Kamanda Msangi amewataka wananchi kutanguliza uzalendo kwanza kuwafichua watu wanaoishi nchini kinyume cha sheria pamoja na kutokuwa na vibali maalumu kwa vyombo vya dola ili kuwakamata na kuwachunguza watu hao.  

ZAIDI YA RAIA SABA WA ETHIOPIA WAMEKAMATWA MKOANI MWANZA. ZAIDI YA RAIA SABA WA ETHIOPIA WAMEKAMATWA MKOANI MWANZA. Reviewed by safina radio on March 05, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.