MAOMBI MAALUM YAMEANDALIWA NA HUDUMA YA REDIO SAFINA ILI KILA MTU KUSIMAMISHA HATI YA KIFO MBELE ZA MUNGU KWA AJILI YA KUONYESHA WATU KUFIA MIGUU YA UKOO.


ARUSHA.

Jamii imeshauriwa kufahamu kuwa baada ya kusimamisha hati inayoonesha kuwa wameshaifia miungu,Yesu Kristo atayakomesha mateso yote yanayo wasumbua kwenye ndoa,uchumi,afya,elimu na changamoto zingine zinazowadhibiti wasimtumikie Mungu kwa Roho na kweli.

Yesu Kristo atayakomesha mateso yote.

Redio safina kesho katika ukumbi wa maombi ulioko Mbauda jijini Arusha kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa sita mchana imeandaa maombi ya maalum ya kila mtu kusimamisha hati ya kifo mbele za Mungu inayoonesha kuwa wameifia miungu ya koo na familia lengo likiwa ni kurudishiwa uzima wa milele wa kutokuharibika.

kuuifia miungu ya koo na familia.
Kwa mujibu wa somo hilo ziko roho,tabia na mienendo ambayo inawatesa watu kama vile mimba kuharibika,kupatwa na magonjwa sugu,kuota ndoto mbaya,migogoro ya ndoa,pamoja na uchumi kuyumba hali ambayo kila mmoja hana budi kusimama na hati ya kifo mbele za Mungu inayoonesha kuwa walishayafia hayo pamoja na Kristo hivyo shetani hapaswi tena kuwatesa.  
Migogoro ya ndoa.
Pia somo hilo limebainisha kuwa zipo baadhi ya dalili zinazoonesha kuwa mtu ameshikiliwa na roho ya miungu kama vile,kuzini kwenye ndoto,kuacha shule bila sababu,kuchanganyikiwa au kufa,kusumbuliwa na ndoto za nyoka,kulishwa vyakula usiku kwenye ndoto,kupitiliza muda muda wa wa kuoa au kuolewa,siku za hedhi,kukandamizwa na roho ya umaskini,pamoja na uchumba kuvunjika.

Siku za hedhi.
Hata hivyo kesho ni siku ya kuondoa roho zote za miungu,magonjwa na matatizo yaliyokuwa yakiwatesa watu kutokana na kushikiliwa na roho ya miungu.

MAOMBI MAALUM YAMEANDALIWA NA HUDUMA YA REDIO SAFINA ILI KILA MTU KUSIMAMISHA HATI YA KIFO MBELE ZA MUNGU KWA AJILI YA KUONYESHA WATU KUFIA MIGUU YA UKOO. MAOMBI MAALUM YAMEANDALIWA NA HUDUMA YA REDIO SAFINA ILI KILA MTU KUSIMAMISHA HATI YA KIFO MBELE ZA MUNGU KWA AJILI YA KUONYESHA WATU KUFIA MIGUU YA UKOO. Reviewed by safina radio on March 02, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.