JUMLA YA FEDHA SHILINGI BILIONI 9.5 ZIMETOLEWA NA SERIKALI KWA UJENZI WA HOSPITALI WILAYANI MOMBA, SONGWE.


SONGWE.

Serikali imetenga jumla ya fedha shilingi bilioni 9.5 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali mpya ya Wilaya ya Momba mkoani Songwe hatua itakayowaondolea wananchi wa wilaya hiyo adha ya kusafiri umbali mrefu kufuata huduma za afya.


Kwa Mujibu wa Mhandisi wa halmashauri ya Tunduma Sospita Lukonja tayari serikali imekwisha kutoa bilioni 2.2 kwa wakala wa majengo Tanzania TBA kwa ajili ya kuanza kwa awamu ya kwanza ya ujenzi wa hospitali hiyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Momba Juma Said ameitaka TBA kukamilisha ujenzi wa hospitali hiyo katika muda uliopangwa na kwa viwango vinavyokubalika.


JUMLA YA FEDHA SHILINGI BILIONI 9.5 ZIMETOLEWA NA SERIKALI KWA UJENZI WA HOSPITALI WILAYANI MOMBA, SONGWE. JUMLA YA FEDHA SHILINGI BILIONI 9.5 ZIMETOLEWA NA SERIKALI KWA UJENZI WA HOSPITALI WILAYANI MOMBA, SONGWE. Reviewed by safina radio on March 02, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.