RAIS WA UGANDA YOWERI MUSEVENI AMFUTA KAZI HENRY TUMUKUNDE NA KALE KAYIHURA KATIKA NYADHIFA ZAO.


KAMPALA.
Rais wa Uganda Yoweri Museveni, amemfuta kazi Inspekta mkuu wa polisi, Kale Kayihura na waziri wa Ulinzi, Henry Tumukunde.

Rais wa Uganda Yoweri Museveni.
Generali Kayihura, ambaye ni mkereketwa wa vita vilivyomsaidia rais Museveni kuingia madarakani mwaka 1986, kwa wakati mmoja alikisiwa kuwa afisa mwenye mamlaka makubwa zaidi katika jeshi la Uganda.
Lakini Generali Kayihura amekuwa akikabiliwa na shinikizo kwa kushindwa kukabiliana na ukosefu wa usalama.
Zaidi ya wanawake 20 wameuawa katika visa vya mauaji ambavyo havijatatuliwa katika maeneo yanayouzunguka mji mkuu wa Kampala, na katika miezi mitatu iliyopita raia watatu wa kigeni pia wameuawa.
Naibu wake Okoth Ochola anashikilia wadhifa huo.
Kwa mujibu wa ujumbe alioandika rais Museveni katika mtandao wa Twitter, amesema kuwa, Kwa uwezo na mamlaka aliliyopewa kikatiba, amemteua Jenerali Elly Tumwiine kama waziri wa usalama,  na  bwana Okoth Ochola kama afisa mkuu wa polisi ambapo Naibu wake atakuwa ni Brigedia Sabiiti Muzeei.
Hata hivyo Mnamo Mei mwaka 2017 Rais Museveni alimteua upya Kayihura kama mkuu wa polisi kwa muhula mwingine wa miaka mitatu,hadi mwaka 2020.

RAIS WA UGANDA YOWERI MUSEVENI AMFUTA KAZI HENRY TUMUKUNDE NA KALE KAYIHURA KATIKA NYADHIFA ZAO. RAIS WA UGANDA YOWERI MUSEVENI AMFUTA KAZI HENRY TUMUKUNDE NA KALE KAYIHURA KATIKA NYADHIFA ZAO. Reviewed by safina radio on March 05, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.