MWIGULU NCHEMBA AWATAKA MADEREVA BODABODA KUIFANYA SHUGHULI YAO KUWA YA HESHIMA, ARUSHA.


ARUSHA.

Waziri wa mambo ya ndani ya nchi Mh. Mwigulu Nchemba amewataka madereva wa bodaboda kuifanya shughuli yao kuwa shughuli ya heshima kwani ni kazi ambayo ina mafanikio kwao na ni sehemu ya utoaji wa huduma kwa jamii.

Waziri wa mambo ya ndani ya nchi Mh. Mwigulu Nchemba.
Mh. Nchemba ameyasema hayo wakati  akizungumza na madereva wa bodaboda  wa jiji la Arusha ambapo amesema kuwa kazi ya kuendesha vyombo hivyo vya moto ni kazi ambayo imetoa fursa kwa vijana wengi hivyo haina budi kuheshimiwa kama kazi nyingine .

Aidha,  amewataka madereva hao kufuata sheria za usalama barabarani ikiwa ni pamoja na kuhakikisha wanakuwa na kofia mbili ngumu  ili kuweza kuepuka ajali zisizo za lazima na upigwaji wa faini kutokana na makaosa ambayo mtu anaweza kukutwa nayo.

Naye,  Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesema kuwa  kutokana na kutokuwepo kwa fursa za mikopo katika benki nyingi, uongozi Mkoa uliweza kuamua kutoa pikipiki 200 kwa Kata 25 huku kila kata ikipewa pikipiki 8 kwa lengo la kuwawezesha vijana kiuchumi na kuweza kujiajiri wenyewe ambapo mpaka sasa zaidi ya  milioni 350 zimesharejeshwa.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Umoja wa madereva wa bodaboda jiji la Arusha Bw. Maulidi Makongoro katika risala yao amesema kuwa umoja huo ulianzishwa  Desemba 2016 kwa lengo la kusimamia shughuli zote za waendesha bodaboda wa jiji la Arusha pamoja na kushughulikia kero na ustawi wa maendeleo yao ambapo mpaka sasa umoja huo una wanachama elfu tano.

MWIGULU NCHEMBA AWATAKA MADEREVA BODABODA KUIFANYA SHUGHULI YAO KUWA YA HESHIMA, ARUSHA. MWIGULU NCHEMBA AWATAKA MADEREVA BODABODA KUIFANYA SHUGHULI YAO KUWA YA HESHIMA, ARUSHA. Reviewed by safina radio on March 05, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.