UMOJA WA MATAIFA UMEIPONGEZA TANZANIA KUTOKANA NA HATUA ZA MAENDELEO INAZOCHUKUA.


KHATOOM.

Umoja wa Mataifa umeipongeza Tanzania chini ya Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Tanzania Rais Dk. John Pombe Magufuli kutokana na hatua za maendeleo inazochukua ambazo zimejengwa na misingi ya amani na utulivu unaochangiwa na Jeshi la Ulinzi na Usalama La Tanzania –JWTZ.

Mwakilishi maalumu wa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia watoto na Migogoro ya Kivita Virginia Gamba akizungumza na Meja Afred Mwinuka wakati alipotembelea kambi ya  Wanajeshi kutoka jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania wanaoshiriki Ulinzi wa Amani chini ya Mpango wa umoja wa mataifa na Umoja wa Afrika UNAMID  Shangilitobaya Jimboni   Darfur Nchini Sudan ( Picha na Luteni Selemani Semunyu).
Pongezi hizo zimetolewa na Mwakilishi Maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia masuala ya watoto na migogoro ya kivita Virginia Gamba wakati wa ziara ya kukagua miradi ya watoto katika vijiji vya Shangitobaya vinavyolindwa na wanajeshi wa Tanzania.

Aidha, amesema kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Venance Mabeyo anapaswa kupongezwa kutokana na mafanikio ya vikosi  vya wanajeshi walioshiriki na wanaoshiriki katika operesheni mbali mbali zikiwemo za umoja wa Mataifa ni kielelezo cha kazi nzuri ya jeshi hilo ndani na nje ya mipaka ya nchi.

Hata hivyo, Mwakilishi huyo wa Katibu Mkuu aliyeambatana  na Viongozi wa Sudan alipata nafasi ya kuzungumza na wanajeshi wa Tanzania katika Kambi ya Shangitobaya kisha kutembelea vituo vya watoto katika kijiji cha Shadayi nchini Sudan.



UMOJA WA MATAIFA UMEIPONGEZA TANZANIA KUTOKANA NA HATUA ZA MAENDELEO INAZOCHUKUA. UMOJA WA MATAIFA UMEIPONGEZA TANZANIA KUTOKANA NA HATUA ZA MAENDELEO INAZOCHUKUA. Reviewed by safina radio on March 05, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.