WASTANI WA MASHAMBULIZI YA 20 YAMEKUWA YAKIFANYWA NA NDEGE ZA JESHI LA URUSI.


WASHINGTON.

Marekani imesema ndege za jeshi la Urusi zimekuwa zikifanya wastani wa mashambulizi 20 kila siku dhidi ya ngome za waasi katika Ghouta ya Mashariki nchini Syria, kati ya tarehe 24 na 28 Februari.

ndege za jeshi za Urusi katika mashambuzi Ghouta Mashariki.
Hiyo ni shutuma kali zaidi kutolewa na Marekani dhidi ya Urusi, ikiihusisha na vifo vya raia katika eneo hilo lililozingirwa.

 Rais wa Syria Bashar al-Assad amesema mashambulizi dhidi ya waasi katika eneo hilo lililo karibu na mji mkuu-Damascus yataendelea.

Akizungumza na  waandishi wa habari jana, Assad amesema usitishaji mapigano wa masaa matano kila siku utaendelea, kutoa fursa kwa raia wanaotaka kuondoka katika eneo hilo kufanya hivyo.

 Rais huyo alikanusha shutuma kwamba jeshi la serikali yake limetumia silaha za sumu, akiziita shutuma hizo kamusi ya uongo ya  nchi za Magharibi.


WASTANI WA MASHAMBULIZI YA 20 YAMEKUWA YAKIFANYWA NA NDEGE ZA JESHI LA URUSI. WASTANI WA MASHAMBULIZI YA 20 YAMEKUWA YAKIFANYWA NA NDEGE ZA JESHI LA URUSI. Reviewed by safina radio on March 05, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.