TANZANIA YAENDELEA KUONYESHA MAFANIKIO MAKUBWA KATIKA NYANJA MBALI MBALI KIMATAIFA HUSUSANI KIUCHUMI.


DODOMA.

Imeelezwa kuwa,Tanzania imeendelea kuonyesha mafanikio makubwa katika Nyanja mbali mbali kimataifa ikiwemo ya ukuaji wa kiuchumi.

Dk. Hassan Abas.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Habari Maelezo ambaye pia ni msemaji wa serikali Dk. Hassan Abas katika ripoti ya mwezi February 2018 iliyotolewa na Shirika la Kimataifa inayoangazia masuala ya Rushwa Transparency International mjini Dodoma.

Taarifa hiyo inaonesha kuwa Tanzania imepanda nafasi 13 duniani katika mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi huku ikishika nafasi ya 2 katika nchi za Afrika Mashariki ikitanguliwa na Rwanda.

Hali kadhalika, Dk. Abas amesema kuwa katika miradi ya kuzalisha umeme wa kinyerezi 1 na 2 imefanikiwa kwa kuwa megawati 240 zinatarajiwa kuzalishwa na Kinyerezi 2.

Hata hivyo, Dk. Abas amezungumzia mambo mengine yanayohusiana na utekelezaji wa miradi mikubwa wa ujenzi wa reli ya kisasa ya Standard Gaurge kutoka Dar es salaam hadi Dodoma na kasi kubwa ya ulipwaji wa madeni ya watumishi na watoa huduma serikali ambapo zaidi ya bilioni 800 kati ya trilioni 1 iliyotengwa na serikali imelipwa.

TANZANIA YAENDELEA KUONYESHA MAFANIKIO MAKUBWA KATIKA NYANJA MBALI MBALI KIMATAIFA HUSUSANI KIUCHUMI. TANZANIA YAENDELEA KUONYESHA MAFANIKIO MAKUBWA KATIKA NYANJA MBALI MBALI KIMATAIFA HUSUSANI KIUCHUMI. Reviewed by safina radio on March 05, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.