ZAIDI YA MADAKTARI 500 WA HOSPITALI YA KENYATTA, KENYA WAMESUSIA KAZI WAKITAKA KUREJESHWA KWA MWENZAO.


NAIROBI.
Zaidi ya madaktari 500 katika hospitali kuu ya Kenyatta nchini Kenya wamesusia kazi wakitaka kurejeshwa kwa mwenzao aliyesimamishwa kazi baada ya kumfanyia kimakosa mgonjwa upasuaji wa kichwa.

Zaidi ya madaktari 500 katika hospitali kuu ya Kenyatta nchini Kenya wamesusia kazi.
Mwenyekiti wa Muungano wa Madaktari nchini, Samuel Oroko, amesema kumsimamisha kazi daktari huyo ilikuwa ni uamuzi ambao hauwezi kutatatua shida zinazoikumba hospitali hiyo.
Muungano huo unataka mfumo mzima wa hospitali kuchunguzwa, ikiwemo kuboresha mfumo wa kunakili data ya wagonjwa na pia kuongezwa kwa idadi ya maeneo ya upasuaji.
Wiki iliyopita, Afisa mkuu mtendaji wa hospitali ya taifa ya Kenyatta mjini Nairobi - Lily Koros - alipewa likizo ya lazima huku Daktari na wahudumu katika hospitali hiyo wakisimamishwa kazi baada ya mgonjwa kufanyiwa upasuaji wa kichwa kimakosa.
Mkasa huo ulitokana na mchanganyiko wa majina ya wagonjwa wawili wote waliokuwa wana matatizo ya kichwa, na kosa halikujulikana hadi mgonjwa mmoja alipopasuliwa kichwa ndani ya chumba cha upasuaji.
Hospitali ya Kenyatta ndio hospitali kubwa zaidi ya umma nchini Kenya, na kusimamishwa kwa shughuli za matibabu huenda kukaathiri shughuli katika hopsitali nyingine nchini humo.
Hata hivyo Takwimu zinaonyesha kuwa hospitali ya Kenyatta huwapokea wagonjwa wasiopungua 3,000 kwa siku.


ZAIDI YA MADAKTARI 500 WA HOSPITALI YA KENYATTA, KENYA WAMESUSIA KAZI WAKITAKA KUREJESHWA KWA MWENZAO. ZAIDI YA MADAKTARI 500 WA HOSPITALI YA KENYATTA, KENYA WAMESUSIA KAZI WAKITAKA KUREJESHWA KWA MWENZAO. Reviewed by safina radio on March 05, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.