BUNGE LA ETHIOPIA LIMEMTEUA ABIYE AHMED KUWA WAZIRI MKUU


Bunge la Ethiopia limemchagua Abiye Ahmed kuwa waziri mkuu wa taifa hilo la pili barani Afrika kuwa na idadi kubwa ya watu kufuatia kuteuliwa kwake na chama tawala wiki iliyopita.

Image result for PICHA YA ABIYE AHMED
ABIYE AHMED

Bw Abiye ameapishwa rasmi leo kuwa Waziri mkuu akimrithi Hailemariam Desalegn ambaye amejiuzulu wadhifa huo kati kati ya mwezi Februari baada ya misururu ya maandamano dhidi ya serikali yaliyosababisha vifo vya mamia ya raia,wengi wao wakiwa ni raia  kutoka maeneo ya Oromia na Amhara.

Waziri Abiye mwenye umri wa miaka 42, ndiye mwanasiasa wa kwanza kutoka jamii ya Oromo kuwa Waziri mkuu huku kukiwa na matumaini kuwa atatuliza maandamano dhidi ya serikali,yaliyozuka tangu mwaka 2015.

Pia ameahidi kuleta mageuzi, kuanzisha mazungumzo na Eritrea na kudokeza kuwa utawala wake utavipa vyama vya kisiasa uhuru zaidi na kuwataka waethiopia walio nje ya nchi kushiriki kikamilifu katika siasa na maendeleo ya nchi.

Waoromo takriban milioni 100, ambao ndiyo wengi zaidi Ethiopia wamekuwa wakilalamika kuwa wanatengwa kisiasa na kiuchumi na utawala.

BUNGE LA ETHIOPIA LIMEMTEUA ABIYE AHMED KUWA WAZIRI MKUU BUNGE LA ETHIOPIA LIMEMTEUA ABIYE AHMED KUWA WAZIRI  MKUU Reviewed by safina radio on April 02, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.