WAZIRI MKUU WA JAPAN SHINZO ABE KUKUTANA NA RAIS TRUMP.


Waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe amesema atakutana na Rais wa Marekani Donald Trump mjini Florida kati ya tarehe 17 hadi 20 mwezi huu kujadili masuala ya biashara, mpango wa kinyuklia na makombora wa Korea Kaskazini pamoja na raia wa Japan wanaoshikiliwa mateka na Korea Kaskazini kwa miongo kadhaa sasa.

Image result for PICHA YA SHINZO ABE WAZIRI MKUU WA JAPAN
WAZIRI MKUU WA JAPAN SHINZO ABE

Bw Abe anapanga kukutana na Trump kabla ya kiongozi huyo wa Marekani kufanya mkutano wa kihistoria na Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un mwishoni mwa mwezi Mei.

Pia amesema kuwa wanahitaji kuendelea na shinikizo dhidi ya Korea Kaskazini ili ichukue hatua madhubuti kuachana na mpango wake wa kinyuklia katika rasi ya Korea.

Mwezi uliopita, Trump aliongeza ushuru dhidi ya bidhaa za bati na chuma zinazoingizwa Marekani kutoka nje huku Japan ikiwa ni miongoni mwa nchi zinazoathirika na ongezeko hilo la ushuru.

WAZIRI MKUU WA JAPAN SHINZO ABE KUKUTANA NA RAIS TRUMP. WAZIRI MKUU WA JAPAN SHINZO ABE KUKUTANA NA RAIS TRUMP. Reviewed by safina radio on April 02, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.