RAIS MAGUFULI AMESEMA KUWA SERIKALI ITAENDELEA KUTEKELEZA MIRADI YA UMEME


Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh John Magufuli amesema kuwa serikali itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya umeme ili kuhakikisha Tanzania inakuwa na umeme wa kutosha.
Image result for PICHA YA RAIS MAGUFULI
RAIS MAGUFULI

Mh magufuli ameyasema hayo leo jijini Dar-es-salaam wakati akizindua mradi wa umeme wa gesi asilia wa Kinyerezi Two wenye thamani ya shilingi bilioni mia saba na hamsini.

Amesema kuwa uchumi wa viwanda unaotarajiwa na serikali hauwezi kufanikiwa bila kuwa na umeme wa uhakika na wa kutosha hivyo jitihada zaidi zinahitajika kufanywa  na serikali ili kuongeza uzalishaji wa umeme kutoka Meg Watts 1400 zinazozalishwa kwa sasa hadi kufikia Mega Watts 5000 kwa siku za baadaye.

Ameongeza kuwa mradi huo aliouzindua leo unatekelezwa na serikali ya Japani kwa kushirikiana na serikali ya Tanzania kwa gharama ya shilingi bilioni mia saba na hamsini na utapunguza kwa kiasi kikubwa upungufu wa umeme hapa nchini.

Kwa upande wake mkurugenzi mkuu wa shirika la umeme hapa nchini Dr Tito Mwinuka amesema kuwa mradi huo utaongeza Mega Watts 240 katika gridi ya Taifa,ambapo pia ameishukuru serikali kwa kutoa fedha na kufanikisha kukamilika kwa mradi huo.

RAIS MAGUFULI AMESEMA KUWA SERIKALI ITAENDELEA KUTEKELEZA MIRADI YA UMEME RAIS MAGUFULI AMESEMA KUWA SERIKALI ITAENDELEA KUTEKELEZA MIRADI YA UMEME Reviewed by safina radio on April 03, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.