WAASI 5 WA BOKO HARAM WAUAWA NCHINI NIGERIA


Jeshi la Nigeria limesema limewaua waasi watano wa kundi la Boko Haram katika jimbo la Borno, kaskazini mashariki mwa Nigeria, na kuwaokoa mateka mia moja arobaini na tisa (149).
Image result for PICHA YA BOKO HARAM


Msemaji wa jeshi la Nigeria Bw. Nwachukwu amesema kuwa  jeshi la Nigeria lilifanya operesheni ya kuwaondoa waasi waliosalia wa kundi la Boko Haram karibu na ngome yake kuu ya zamani iliyoko kwenye msitu wa Sambisa.

Aidha, Bw. Nwachukwu amesema kuwa katika operesheni hiyo wamewaua waasi watano  na wengine watano wamekamatwa na mateka mia moja arobaini na tisa (149) wameokolewa.

Hata hivyo, msemaji huyo ameongeza kuwa kati ya mateka hao 149 kuna wanawake 54 na watoto 95, ambao hivi sasa wamepelekwa katika kituo cha afya kwa ajili ya matibabu.

WAASI 5 WA BOKO HARAM WAUAWA NCHINI NIGERIA WAASI 5 WA BOKO HARAM WAUAWA NCHINI NIGERIA Reviewed by safina radio on April 09, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.