DK. MWAKYEMBE AWATAKAMAAFISA HABARI NCHINI KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO KWA MUJIBU WA SHERIA, KANUNI, NA TARATIBU ILI KUONESHA WELEDI WA KAZI ZAO.
ARUSHA.
Waziri wa Habari habari, sanaa, utamaduni na michezo
Dk.Herson Mwakyembe amewataka maafisa habari nchini kutekeleza
majukumu yao kwa mujibu wa sheria, kanuni na utaratibu ili kuonesha weledi
wakazi zao.
Akifungua kikao kazi cha 14 cha maafisa habari, mawasiliano na mahusiano, mkoani Arusha leo Dk. Mwakyembe ametoa maagizo kwa maafisa hao kuwa baada ya mkutano huo unaotarajiwa kudumu kwa siku tano na kumalizika ni wajibu wa kila mshiriki kufanya kazi kwa mujibu wa sheria ambapo amesema watakaokiuka hatua za kisheria zitafuatwa.
Aidha, Amesema kuwa wapo maafisa habari wazembe wasiojishughulisha na kutafuta habari za wizara, taasisi na kusubiri hadi taasisi itangaze kuwepo kwa mkutano, ziara na mambo kama hayo jambo alilosema ni uzembe na kudhalilisha taaluma huku akiwataka kwenda na wakati kutoa habari za taasisi,Halmashauri kila Mara ili kuhabarisha umma na serikali kwa ujumla.
Akifungua kikao kazi cha 14 cha maafisa habari, mawasiliano na mahusiano, mkoani Arusha leo Dk. Mwakyembe ametoa maagizo kwa maafisa hao kuwa baada ya mkutano huo unaotarajiwa kudumu kwa siku tano na kumalizika ni wajibu wa kila mshiriki kufanya kazi kwa mujibu wa sheria ambapo amesema watakaokiuka hatua za kisheria zitafuatwa.
Aidha, Amesema kuwa wapo maafisa habari wazembe wasiojishughulisha na kutafuta habari za wizara, taasisi na kusubiri hadi taasisi itangaze kuwepo kwa mkutano, ziara na mambo kama hayo jambo alilosema ni uzembe na kudhalilisha taaluma huku akiwataka kwenda na wakati kutoa habari za taasisi,Halmashauri kila Mara ili kuhabarisha umma na serikali kwa ujumla.
Amewataka pia kujenga ushirikiano mzuri baina yao na vyombo vya habari vilivyo wazunguka ili kuhakikisha taarifa zinafikia umma ambapo amesema siyo kila taarifa ni taarifa ya kutoa bali zile zilizosahihi ambapo ushirikiano kati ya vyombo vya habari na Maafisa hao utafanya kufikisha taarifa sahihi.
Pia, Amezitaka wizara, Halmashauri, pamoja na taasisi kuwapatia vifaa vya kazi maafisa habari ili waweze kutekeleza majukumu kwa urahisi ambapo amesema kama wizara au taasisi haziwapatii vifaa hiyo ni changamoto na taasisi, wizara hizo zitakuwa tatizo.
Naye mwenyekiti wa chama cha maafis mawasiliano serikalini
(TAGCO) Pascal Shelutete amesema lengo la kuanzishwa kwa Chama hicho ni
pamoja na kuhakikisha inaendeleza tasnia ya mawasiliano katika weledi
unaotakiwa kwa wanatasnia wote kutoka serikali kuu hadi serikali za
mitaa.
Kwa upande wa mwakilishi wa Umoja wa mataifa Alvaro Rodriguez amesema Umoja wa mataifa unapenda kuwa washirika wa serikali katika mawasiliano ya maendeleo nchini kwa kuwa nao ni watumishi wa umma.
Hata hivyo kauli mbiu ya mkutano huo wa maafisa habari,mawasiliano,Mahusiano na itifaki ni ' Je Mawasiliano ya kimkakati yanachangiza vipi Tanzania ya viwanda'
Kwa upande wa mwakilishi wa Umoja wa mataifa Alvaro Rodriguez amesema Umoja wa mataifa unapenda kuwa washirika wa serikali katika mawasiliano ya maendeleo nchini kwa kuwa nao ni watumishi wa umma.
Hata hivyo kauli mbiu ya mkutano huo wa maafisa habari,mawasiliano,Mahusiano na itifaki ni ' Je Mawasiliano ya kimkakati yanachangiza vipi Tanzania ya viwanda'
DK. MWAKYEMBE AWATAKAMAAFISA HABARI NCHINI KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO KWA MUJIBU WA SHERIA, KANUNI, NA TARATIBU ILI KUONESHA WELEDI WA KAZI ZAO.
Reviewed by safina radio
on
March 12, 2018
Rating:
No comments