DOLA BILIONI 1.7 ZATARAJIWA KUCHANGISHWA NA WAFADHILI MBALIMBALI ILI KUFANIKISHA MISAADA YA KIBINADAMU.


KINSHASA.
Wafadhili mbalimbali wanatarajiwa kukutana mwezi ujao kuchangisha Dola Bilioni 1.7 ili kufanikisha misaada ya kibinadamu kuwasaidia mamilioni ya wakimbizi nchini DRC.

Umoja wa Mataifa.
Hatua hiyo imetangazwa na Umoja wa Mataifa, ambao umesema unahitaji fedha hizo kufanikisha miradi yake katika taifa hilo ambalo limekumbwa na ukosefu wa usalama eneo la mashariki hasa katika jimbo la Kasai.
Mkutano huo umepangwa kufanyika tarehe 13 mwezi ujao jijini Geneva nchini Uswisi.
Wiki mbili zilizopita Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia Wakimbizi (UNHCR) lilisema kuwa vurugu zinazoendelea kuongezeka katika mkoa wa kusini mashariki mwa Tanganyika nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) zinachochea maafa ya kutisha ya kibinadamu.
Katika majuma mawili ya kwanza ya mwezi Februari, mashirika yanayoshirikiana na UNHCR yaliorodhesha matukio mia nane, ikiwa ni pamoja na mauaji, utekaji nyara na ubakaji huku vurugu nyingi zikitajwa kufanyika katika maeneo ambayo ni vigumu kwa wafanyakazi wa kibinadamu kufika.

DOLA BILIONI 1.7 ZATARAJIWA KUCHANGISHWA NA WAFADHILI MBALIMBALI ILI KUFANIKISHA MISAADA YA KIBINADAMU. DOLA BILIONI 1.7 ZATARAJIWA KUCHANGISHWA NA WAFADHILI MBALIMBALI ILI KUFANIKISHA MISAADA YA KIBINADAMU. Reviewed by safina radio on March 02, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.