KIKOSI KAZI CHAUNDWA NA JESHI LA POLISI MKOA WA PWANI ILI KUFUATILIA MADEREVA WANAOWASHAWISHI ASKARI KUPOKEA RUSHWA.


PWANI.

Jeshi la polisi mkoani Pwani limeanzisha kikosi kazi maalumu kwa ajili ya kufuatilia madereva wanaowashawishi askari wao kupokea rushwa pindi wanapokutwa na makosa mbalimbali ya usalama barabarani.


Hayo yameelezwa na kamanda wa jeshi la polisi mkoani Pwani Jonathan Shana wakati akizungumza na waandishi wa habari mkoani humo,ambapo amesema kuwa jeshi hilo litawapandisha vyeo askari watakao wakamata madereva wanaojaribu kuwashawishi wapokee rushwa.

Kamanda Shana amesema kuwa mkakati huo ni mojawapo wa kupambana na ajali za barabarani mkoani Pwani.

Ameongeza kuwa kikosi kazi hicho kilichoundwa na makachero kimeshaanza kazi na hatua za kisheria zitachukuliwa mara moja kwa madereva watakaokutwa na makosa hayo ikiwa ni pamoja na kufikishwa mahakamani.

Hata hivyo mkakati huo unalenga kuwafungia leseni na pia kutangaza kwenye vyombo vya habari makampuni yote ya mabasi ambayo yatakuwa yamekithiri kwa makosa ya mwendo kasi.

KIKOSI KAZI CHAUNDWA NA JESHI LA POLISI MKOA WA PWANI ILI KUFUATILIA MADEREVA WANAOWASHAWISHI ASKARI KUPOKEA RUSHWA. KIKOSI KAZI CHAUNDWA NA JESHI LA POLISI MKOA WA PWANI ILI KUFUATILIA MADEREVA WANAOWASHAWISHI ASKARI KUPOKEA RUSHWA. Reviewed by safina radio on March 02, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.