WAKULIMA WA KANDA YA KASKAZINI WATAKIWA KUFUA UTABIRI WAHALI YA HEWA UNAOTOLEWA NA MAMLAKA YA HALI YA HEWA.


ARUSHA.

Wakazi wa kanda ya Kaskazini hususani wakulima wametakiwa kufuatilia utabiri wa hali ya hewa unaotolewa na mamlaka ya hali ya hewa hapa nchini ili waweze kukabiliana na majanga mbalimbali yanayosababishwa na mbadiliko ya tabia nchi.

Wito huo umetolewa na mtaalamu wa mamlaka hiyo mkoa wa Arusha Bw Justice Kijazi wakati akizungumza na Redio Safina kuhusu kuanza kwa mvua za masika kwa mwaka huu wa 2018.

Bw Kijazi amesema kuwa ikiwa wakulima  watafuatilia utabiri wa hali ya hewa itawasaidia kuandaa mashamba yao mapema pamoja na kujua ni mazao gani wanaopaswa kupanda na katika ukanda upi ili wasije kupata hasara na kukabiliana na baa la njaa.

Amesema kuwa kwa mwaka huu wa 2018 katika mikoa ya kanda ya Kaskazini ya Kilimanjaro,Arusha na Manyara mvua za masika zitaanza kunyesha wiki ya pili ya mwezi March na zinatarajiwa kukatika wiki ya tatu ya mwezi Mei hivyo ni vyema wakafuatilia utabiri huo ili waanze kilimo chao kwa wakati.

Hata hivyo ameongeza kuwa ili kuhakikisha mkulima anafahamu umuhimu wa kufuatilia utabiri wa hali hewa wamekuwa wakitoa elimu kwa njia mbalimbali ikiwemo Televisheni,Redio,na majarida mbalimbali.

WAKULIMA WA KANDA YA KASKAZINI WATAKIWA KUFUA UTABIRI WAHALI YA HEWA UNAOTOLEWA NA MAMLAKA YA HALI YA HEWA. WAKULIMA WA KANDA YA KASKAZINI WATAKIWA KUFUA UTABIRI WAHALI YA HEWA UNAOTOLEWA NA MAMLAKA YA HALI YA HEWA. Reviewed by safina radio on March 02, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.