JAE-IN APANGA KUTUMA MJUMBE MAALUMU KWENDA KOREA KASKAZINI.


SEOUL.
Rais wa Korea kusini Moon Jae-in anapanga kutuma mjumbe maalum kwenda Korea kaskazini hivi karibuni kutayarisha mazungumzo yatakayokuwa na maana zaidi kati ya mataifa hayo hasimu.

Moon Jae-in Rais wa Korea kusini.
Korea kusini ina matumaini kuwa mazungumzo hayo hatimaye yatajumuisha majadiliano kuhusiana na Korea kaskazini kuachana na mpango wake wa silaha za kinyuklia.

 Ofisi ya rais wa Korea kusini imesema Moon amewasilisha mpango huo kwa rais Donald Trump katika mazungumzo ya simu ya dakika 30 jana Alhamisi ambapo ofisi hiyo haikusema Trump alichukuliaje hatua hiyo.

Maafisa wa Korea kaskazini waliotembelea Korea kusini kwa ajili ya michezo ya Olimpiki ya majira ya baridi mjini Pyeongchang hivi karibuni wamesema kiongozi wao Kim Jong Un anataka kufanya mkutano wa kilele na Moon na kwamba Korea kaskazini inapanga kuanzisha mazungumzo na Marekani.

JAE-IN APANGA KUTUMA MJUMBE MAALUMU KWENDA KOREA KASKAZINI. JAE-IN APANGA KUTUMA MJUMBE MAALUMU KWENDA KOREA KASKAZINI. Reviewed by safina radio on March 02, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.