WAGOMBEA ITALIA WAPATA FURSA YAO YA MWISHO KUWAVUTIA WAPIGA KURA HII LEO.

ROME.

Kampeni za uchaguzi nchini Italia uliopangwa kufanyika tarehe 4 Jumapili zinamalizika leo.
Silvio Berlusconi 
Silvio Berlusconi pamoja na wagombea wengine katika uchaguzi huo ambao hautabiriki wanapata fursa yao ya mwisho kuwavutia wapiga kura hii leo.

Berlusconi anaongoza muungano wa vyama vya mrengo wa kulia ambao unatarajia kupata ushindi dhidi ya vuguvugu la kupinga utawala wa Five Star (M5S) pamoja na chama tawala cha siasa za wastani za mrengo wa kushoto cha Democraric DP, lakini muungano wa vyama hivyo hauna hakika ya kupata wingi wa viti katika bunge.

Berlusconi mwenye umri wa miaka 81 ambaye aliwahi kuwa waziri mkuu wa Italia amekuwa akifanya mahojiano ya televisheni na redio tu na kujiweka mbali na heka heka za kampeni za kwenda huku na huko.

WAGOMBEA ITALIA WAPATA FURSA YAO YA MWISHO KUWAVUTIA WAPIGA KURA HII LEO. WAGOMBEA ITALIA WAPATA FURSA YAO YA MWISHO KUWAVUTIA WAPIGA KURA HII LEO. Reviewed by safina radio on March 02, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.