HALMASHAURI YA WILAYA YA MERU INATARAJIA KUPITIA BAJETI YAKE KUTOKANA AGIZO LA WAZIRI JAFFO.


ARUSHA

Kufuatia agizo lililotolewa na waziri wa nchi ofisi ya Rais Tawala za mikoa,na serikali za mitaa TAMISEMI Mh suleman Jaffo kwa wenyeviti wa halmashauri nchi nzima kupitia bageti zao upya, halmashauri ya Meru inatarajia kupitia bageti yake kwa kutoa vipaumbele katika elimu na sekta ya Afya.
Mh suleman Jaffo 
Akizungumza na Safina Redio ofisini kwake wilayani Arumeru mwenyekiti wa halmashauri ya Meru Wille Njau amesema kuwa kutokana na agizo hilo la Mh waziri halmashauri yake itachagua na kutekeleza miradi itakayoleta manufaa kwa wananchi.

Aidha mwenyekiti huyo amesema moja kati ya mambo watakayotoa kipaumbele wakati wa kupitia bageti hiyo ni pamoja na mradi wa shule za sekondari ikiwemo shule ya sekondari  Uwiro na Nansio pamoja na vituo vya afya na zahanati ambazo hazijakamilika.

Katika hatua nyingine mwenyekiti huyo  amewataka wakulima kuandaa mashamba mapema ili kupanda mazao yao kwa wakati na hiyo itawasaidia kuepukana na janga la njaa.

HALMASHAURI YA WILAYA YA MERU INATARAJIA KUPITIA BAJETI YAKE KUTOKANA AGIZO LA WAZIRI JAFFO. HALMASHAURI YA WILAYA YA MERU INATARAJIA KUPITIA BAJETI YAKE KUTOKANA AGIZO LA WAZIRI JAFFO. Reviewed by safina radio on March 01, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.