HUDUMA YA REDIO SAFINA IMEANDAA MAOMBI MAALUMU YA KUVUSHWA MIPAKA KWA MTU PAMOJA NA KUSHUGHULIKIA WACHAWI NA WAGANGA WA KIENYEJI AMBAO WAMEKUWA KIAMBAZA KATIKA MAFANIKIO YA WENGI.


ARUSHA.

Imebainishwa kuwa upo uwezekano mkubwa wa wachawi na waganga wa kienyeji kukamata ufahamu wa mtu na kumfanya kushindwa kufanya jambo lolote la msingi kwasababu ya kuwekewa mipaka kiroho na kimwili kwa njia za ushirikina.

Huduma ya redioa safina kesho katika ukumbi wa maombi uliopo mbauda jijini Arusha kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa sita na nusu mchana imekuandalia maombi maalumu ya kuvushwa mipaka ikiwa ni pamoja na kuwashughulikia wachawi na wanganga wa kienyeji ambao wamekuwa kiambaza katika mafanikio ya wengi.

Aidha wapo baadhi ya watu ambao wameshindwa kutambua majira na nyakati sahihi za wao kufanya biashara,kulima,kufuga,kusoma,kuoa au kuolewa kutokana majira na nyakati zao kukamatwa na wachawi na hatimae kuishia kuwa watu wasiokuwa na makao katika jamii baada ya adui kuwawekea mipaka.

Kutokana na watu kuwekewa mipaka pamoja na kukamatwa ufahamu hadi kushindwa kujishughulisha na kazi yoyote ya kuwapatia kipato baadhi ya watu wamekuwa wavivu, ombaomba,walevi,wezi,na masikini hali inayowafanya wengi kuwa mzigo katika jamii na Taifa kwa ujumla.

Hata hivyo kesho katika ukumbi wa maombi uliopo mbauda jijini Arusha mahitaji mbalimbali yataombewa sambamba na maombi ya kuwapinga wachawi na waganga wakienyeji ili waweze kuwaachilia watu waweze kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine kiuchumi na kiroho.



HUDUMA YA REDIO SAFINA IMEANDAA MAOMBI MAALUMU YA KUVUSHWA MIPAKA KWA MTU PAMOJA NA KUSHUGHULIKIA WACHAWI NA WAGANGA WA KIENYEJI AMBAO WAMEKUWA KIAMBAZA KATIKA MAFANIKIO YA WENGI. HUDUMA YA REDIO SAFINA IMEANDAA MAOMBI MAALUMU YA KUVUSHWA MIPAKA KWA MTU PAMOJA NA KUSHUGHULIKIA WACHAWI NA WAGANGA WA KIENYEJI AMBAO WAMEKUWA KIAMBAZA KATIKA MAFANIKIO YA WENGI. Reviewed by safina radio on March 12, 2018 Rating: 5

No comments