ZAIDI YA EKARI TATU ZA BANGI ZACHOMWA MOTO MAISOME , WILAYANI SENGEREMA MKOANI MWANZA.


MWANZA.

Zaidi ya Ekari tatu za bangi zimeteketezwa ndani ya hifadhi ya msitu wa  Maisome katka kisiwa cha Maisome wilayani Sengerema mkoani Mwanza.

Hayo yamesemwa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Sengerema Bw. Anne Mhina ambapo amesema zao hilo limelimwa katika sehemu ya Msitu huo wenye ukubwa wa hekta elfu kumi na mbili na mia nane.

Aidha, amesema kuwa bangi hiyo imeteketezwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo katika operesheni maalumu ya kukomesha kilimo cha zao hilo haramu.

Pia, amesema kuwa mikakati yao ni kukomesha kilimo hicho,na kuwatafuta wanaolima zao hilo pamoja na mashamaba ya wakulima yaliyooteshwa zao hilo ili kuyavuna na kuyateketeza.

Kwa upande wake Meneja wa Wakala Misitu Tanzania TFS wilaya ya Sengerema Bw. Urio Jeremaya amesesma kuwa mbali na hilo operesheni hiyo imelenga kukomesha shughuli nyingine za kibinadamu zinazotishia uhai wa hifadhi hiyo.

ZAIDI YA EKARI TATU ZA BANGI ZACHOMWA MOTO MAISOME , WILAYANI SENGEREMA MKOANI MWANZA. ZAIDI YA EKARI TATU ZA BANGI ZACHOMWA MOTO MAISOME , WILAYANI SENGEREMA MKOANI MWANZA. Reviewed by safina radio on March 12, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.