NDEGE YA ABIRIA 67 IMEANGUKA WAKATI IKITUA INCHINI NEPAL.
KATHMANDU.
Ndege ya
abiria kutoka Bangladesh iliyokuwa na abiria 67 imeanguka wakati ikitua katika
Uwanja wa Kimataifa wa ndege wa Kathmandu nchini Nepal nakuua watu kadhaa.
Maafisa
nchini Nepal wanasema kuwa abiria 17 kati ya 67 ndio waliookolewa huku wengine
wakisadikiwa kupoteza maisha.
Habari
zinaeleza kuwa ndege hiyo ilikuwa ikiitokea jijini Dhaka, kuelekea jijini
Kathmandu.
Moto mkubwa
na moshi mzito ulishuhudiwa wakati ndege hiyo ilipoanguka ambapo maafisa
wamekuwa wakiendelea na zoezi la kuuzima
ili kuona iwapo wataweza kuwaokoa abiria
wengine.
Hata hivyo
uchunguzi unaendelea ili kubaini chanzo cha ajali ya ndege hiyo inayomilikiwa
na kampuni ya Marekani, US-Bangla.
NDEGE YA ABIRIA 67 IMEANGUKA WAKATI IKITUA INCHINI NEPAL.
Reviewed by safina radio
on
March 12, 2018
Rating:
No comments