OLF LIMEKUWA TISHIO KWA JESHI LA ETHIOPIA .


ADDIS ABABA.
Jeshi la Ethiopia limeanzisha uchunguzi kubaini namna raia 9 walivyouawa na wengine 12 kujeruhiwa baada ya kushambuliwa kimakosa katika eneo la Moyale katika mpaka wa nchi hiyo na Kenya.
Ripoti zinasema kuwa wanajeshi kadhaa wamesimishwa kazi, baada ya kuwaua raia hao wakati wa makabiliano na waasi.
Jeshi la Ethiopia kwa muda mrefu sasa, limekuwa likipambana na waasi wanaojiita Oromo Liberation Front (OLF) ambao serikali ya Addis Ababa inasema ni magaidi na wanatishia usalama wa nchi hiyo.
Ethiopia imekuwa ikikabiliwa na changamoto za kiusalama tangu mwaka 2016, baada ya maandamano kutoka majimbo ya Oromia na Amhara.
Wakaazi wa majimbo hayo mawili, yanaishtumu serikali ya Ethiopia kwa kuwatenga kimaendeleo hali iliyomsababisha Waziri Mkuu Hailemariam Desalegn, kujiuzulu huku hali ya hatari ikitangazwa kwa muda wa miezi sita.

OLF LIMEKUWA TISHIO KWA JESHI LA ETHIOPIA . OLF LIMEKUWA TISHIO KWA JESHI LA ETHIOPIA . Reviewed by safina radio on March 12, 2018 Rating: 5

No comments